Mkutano Mkuu wa Jumu...
Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Zigi Chini (WUA-JUWAMAZICHI)
09 Jan, 2026 1:30AM-10:30PM Ukumbi wa Amboni -Ofisi ya Mkurugenzi wa Jiji la Tanga
Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Watumia Maji Mto Zigi Chini (WUA-JUWAMAZICHI)

Mkutano Mkuu wa Jumuiya ya Watumia Maji Zigi Chini (WUA-JUWAMAZICHI) umefanyika  tarehe 14/1/2026 katika Ukumbi ya Amboni Caves  uliopo katika Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Jiji la Tanga ambapo watumia maji kwa maana ya wanachama kutoka katika makundi mbalimbali ya Wakulima, Wafugaji, Wadau wa uhifadhi wa Mazingira, Wavuvi, Maji majumbani, Viwanda, Taasisi za Kijamii na wadau mbalimbali walishiriki. Mkutano ulifunguliwa na Mkuu wa Wilaya ya Tanga Mhe. Dadi Kolimba.

Jumuiya hii ya Watumia Maji ya Mto Zigi Chini ni mojawapo ya Jumuiya 24 zilizoanzishwa na kusajiliwa na Bonde la Pangani tangia mwaka 2016 na kupewa Namba ya Usajili 11400013. Kuanzia wakati huo Jumuiya hii imekuwa ikitekeleza majukumu yake ya Usimamizi wa Rasilimali za Maji kwenye eneo lake kwa mujibu wa Sheria na taratibu mbalimbali walizojiwekea kwenye Katiba ya Jumuiya. Eneo hilo la Jumuiya linajumuisha Halmashauri 3 za Tanga Jiji, Mkinga na Muheza. Tarafa 3 za Maramba, Ngomeni na Chumbageni. Kata 7 za Mnyenzani, Gombero, Mabokweni, Mzizima, Kiomoni, Pande Darajani na Mhinduro pamoja na Vijiji/ Mitaa 24. Katika kutekeleza majukumu yake na kwa kuzingatia ukubwa wa eneo hili ambalo Jumuiya hii inalisimamia, imekuwa ikishirikiana na wadau mbalimbali kama vile Halmashauri za Wilaya, Ofisi za Wakuu wa Wilaya, Mamlaka ya Maji-TANGAUWASA, RUWASA, Wadau kutoka Shirika la Maendeleo ya Ujerumani-GIZ, TFS, Marine Park, DoCG, Bandari ya Tanga, Kampuni ya KT Link, Kampuni ya MeTL, EACOP, Ofisi za Tarafa, Kata na Vijiji/Tarafa, Vyombo vya Habari, Wanahabari pamoja na wadau wengine.

Lengo la Mkutano huo ulikuwa ni kufanya uchaguzi  wa Viongozi wa Kamati Tendaji  ya Jumuiya pamoja na Wawakilishi wa Kanda za Mto Zigi Chini watakaodumu madarakani kwa kipindi cha Miaka mitatu (3). Viongozi wa Kamati Tendaji ya Wajumbe 6 waliochaguliwa ni Ndugu Cosmass Chilulumo, Mwenyekiti Msaidizi-Yohana Ruwa, Katibu-Maiko Peter Guni, Mhazini-Bi. Hadija Hassan na Wajumbe 2 Bi. Saumu Jihada na Bi. Abigaeli Ibrahim.

Viongozi hao watakuwa na majukumu ya kujenga na kuimarisha ushirikiano baina ya watumia maji katika kulinda na kuhifadhi vyanzo vya maji na mazingira ndani ya eneo la MtO Zigi Chini na kuhakikisha maji yanatumika kwa usawa na haki.

'UTUNZAJI WA VYANZO VYA MAJI NI JUKUMU LETU SOTE'